Kiosk miongozo ya masomo

Hata kama wewe si mwenye akilli maalum, unaweza kutumia maarifa kama yale ya Aristotle na Einstein ili kuongoza vizuri zaidi wakati wako ujao.

Kujitayarisha kujifunza

Kufikiria kama mwenye akili maalumu

Maarifa yafuatao nane yanaweza kukutia moyo uwe na kufikiria kwenye matunda ili uweze kupata ufumbuzi wa matatizo mbali mbali.

Maarifa haya ni ya kawaida kwa mtindo wa kufikiria na wenye akili maalum hasa katika sayansi, sanaa na kazi ya viwanda."

1. Angalia matatizo katika njia mbali mbali,
na upate ile njia yenye haijatumiwa na mtu yeyote.

Leonardo da Vinci aliamini kwamba, kupata maarifa ya umbo wa matatizo, huaanza na kujifunza kuratibisha upya matatizo katika njia mbali mbali.

2. Wazia!

Einstein alipofikiria juu ya tatizo, alifikiria katika njia nyingi pamoja na kutumia picha za kueleleza. Aliwazia ufumbuzi na aliamini kwamba maneno na hesabu( namba) havikusaidia kufikiria kwake.

3. Kuwa na mazao!
Mazao ndio tabia ya kupambanua wale wenye akili maalumu.

Thomas Edison alijitoa kwa kazi yake. Alipofanya utafiti kati ya wasayansi 2,036, Dean Keith Simonton wa chuo kikuu cha California alipata kwamba msayansi alishemiwa sana hakuzaa tu kazi nzuri, pia kazi "mbaya". Wasayansi hawakuwa na uwoga wa kukosa ili kupata.

4. Tengeneza michanganyiko mipya.
Changanya na kuchanganya, mawazo, picha za mawazoni, katika michanganyiko mbali mbali bila kujali vile itatoka.

Sheria za ufananaji wa mtoto na wazazi wake ambazo ni msingi wa sayansi ya kisasa zilitoka kwa Austrian monk Grego Mendel, ambaye alichanganya elimu ya hesabu na elimu ya viumbe.

5. Tengeneza mahusiano;
tengeneza mahusioano kati ya visa ambavyo si sawa.

Da Vinci alishurutisha uhusiano kati ya sauti ya kengele na jiwe kupiga maji. Hii ilimsaidia kujua kwamba sauti usafiri ndani ya maji. Samuel Morse alivumbua vituo vya kupokea na kupeleka ishara za simu alipotazama vituo vya kupokea na kupeleka vya farasi.

6. Fikiria kwa njia ya kinyume

Msayansi Niels Bohr aliamini kwamba, ukiweka pamoja mambo yalio kinyume, akili zako zinapelekwa jukwaa mpya.

7. Fikiria kwa njia ya mifano

Aristotle alifikiri kuwa mfano ni ishara ya kuwa na akili maalumu, na akaamini kwamba mtu aliyekuwa na uwezo wa kulinganisha mambo mawili yaliofanana, huyo mtu alikuwa mjaliwa wa vipawa maalum. 

8. Jitayarishe, unaweza kuwa na bahati.

Tunapojaribu kufanya jambo na tunashindwa, tunafanya jambo tofauti. Hiyo ni kanuni ya kwanza ya uumbaji wa kiajali. Kushindwa kunaweza kuwa na mazao tusipokaza macho kutokuwa na matokeo. Usijiulize, "ni kwa nini nilishindwa?" Badala, changanua njia ya kufuatwa, sehemu maalum na vile unaweza kuzibadilisha upate matokeo.

Kuendekeza na ruhusa kutoka kwa: Michalko, Michael, Kufikiria kama mwenye akili maalum: Maarifa nane ya uumbaji kutoka kwa Aristotle na Leonardo kwa Einstein na Edison(New Horizons for Learning) vile yanaokena katika http://www.newhorizons.org/wwart_michalko1.html, (June 15, 1999) Makala haya yalionekana kwa mara ya kwnanza ndani ya THE FUTURIST, Mei 1998
Michael Michalko ndiye mwandidhi wa Thinkertoys (Kijitabu cha shughuli za uumbaji), ThinkPak (A Brainstorming Card Set), na Cracking Creativity: The Secrets of Creative Geniuses (Ten Speed Press, 1998).
Tazama pia:

Kujifunza Kupata habari | Jinsi Ya Kushughulika na Mkazo |
Kufikiria kama mwenye akili maalumu