Kiosk miongozo ya masomo

Wanajua mengi wale wanajua kujifunza
Henry Brooks Adams

Mwongozo wa kujifunza

Kujitayarisha kujifunza

Kujifunza Kusoma

Njia ya kujifunza kunaofaa ni

  • kujijua wewe mwenyewe
  • kujua ujazo wako wa kujifunza
  • kujua njia umetumia hapo zamani na ukafaulu
  • kujua kivuta moyo na maarifaa ya jambo unalotaka kujifunza

Inaweza kuwa rahisi kujifunza Phisikia lakini iwe vigumu kujifunza "tennis".
Aina zote za kujifunza hufuata hatua fulani.

Hizi ndizo hatua nne za kujifunza.
Anza kwa kujibu maswali yafuatayo.
Ndipo upange maarifa yako na majibu yako pamoja na
"miongozo mingine ya kujifunza"

Anza na yale
yaliopita

Ulipata ujuzi gani kuhusu habari na jinsi unavyojifunza?
Je,

  • Ulipenda kusoma? Ulifumbua matatizo? Ulijifunza kwa moyo? ulisimulia? ulifasiri? ulunena kwa makundi?
  • ulijua kufupisha?
  • uliuliza maswali kuhusu ulichojifunza?
  • ulikagua?
  • uliweza kufikia namna nyingi za asili ya habari?
  • ulipenda kujifunza peke yako au kwa makundi?
  • uliitaji vipindi vingi vya kujifunza au kikundi kimoja kirefu?

Mazoeo yako ya kujifunza ni yapi? ulipataje mazoeo yako? Zoeo lipi lilikuwa bora zaidi?Zoeo lipi lilikuwa baya zaidi?

Uliweza kueleza kwa njia gani kile ulichifunza bora zaidi? Kwa kufanya majaribio yalioandikwa au kuonana kwa habari fulani?

Endelea na ya sasa ( ya leo)

Nimevutwa moyo kiasi gani na ya sasa?
Ni wakati kiasi gani ninataka kutumia kijifunza haya?
Ni nini kinaoshindana na usikivu wangu?

 

Jiulize kama hali iko sawasawa kwa kufaulu?
Ni nini naweza kukitawala na nini sitaweza kikitawala?
Naweza kubadilisha mankili hizi kwa kufaulu?

Nini chageuza kujitolea kwangu kuyasoma haya?

Ninao mpango? Je, mpango wangu hufikiria ujuzi wangu wa zamani na mtindo wa elimu?

Fikiria njia ya kufuatwa pamoja na jambo unaloliangalia

Ni lipi neno kuu?
Ni maneno yapi yanaosikika kushinda mengine?
Ninayaelewa?

 

Ni nini ninachokijua kuhusu mambo hili?
Je, ninajua mambo yanao uhusiano na mambo haya?

Namna gani za habari zitanisaidia?
Je, nitategemea asili moja tu (kwa mfano, kitabu cha mafundisho) kwa kupata habari?
Itanibidi nitafute asili nyingine zaidi?

Ninapojifunza, ninajiuliza kama ninaelewa?
Nisome kwa upesi au polepole?
Kama sielewi, ninajiuliza ni kwa sababu gani?

Je, ninakoma na kufupisha ninayoyasoma?
Ninakoma na kujiuliza kama ufupisho wangu ni wenye maana dhahiri?
Ninakoma na kuangalia kama ninakubaliana au ni kutopatana?

Ninahitaji wakati wa kufikiria na kulirudia hili jambo baadaye?
Nahitaji kulizungumzia hili jambo na wanafunzi wengine ili nieweze kuelewa vizuri habari hii?
Ninahitaji mjuzi wa habari fulani kama mwalimu au mtunza vitabu?

Fanya
Ukaguzi

Nini nilichokifanya sawasawa?
Nini ningekifanya vizuri zaidi?
Mpango wangu ulienda sawa na wakati kulingana na nguvu na udhaifu wangu?

 

Je, nilichagua hali nzuri?
Nilikuwa na nidhamu?

Nilifaulu?
Nilisherekea kufaulu kwangu?


Tazama pia:

Kujifunza Kupata habari | Jinsi Ya Kushughulika na Mkazo |
Kufikiria kama mwenye akili maalumu